4 Jina la Yesu, salamu!


1. Jina la Yesu, Salamu!
Lisujudieni,
Ninyi Mbinguni, hukumu
Na enzi mpeni.
 
2. Enzi na apewe kwetu,
Watetea dini;
Mkuzeni Bwana wenu,
Na enzi mpeni.
 
3. Enyi mbegu ya rehema,
Nanyi msifuni;
Mmeponywa kwa neema,
Na enzi mpeni.
 
4. Wenye dhambi kumbukeni
Ya msalabani,
Kwa furaha msifuni,
Na enzi mpeni.
 
5. Kila mtu duniani
Msujudieni,
Kote-kote msifuni,
Na enzi mpeni.
 
6. Sisi na wao pamoja
Tu mumo sifani,
Milele sifa ni moja,
Ni “Enzi mpeni.” 

Comments

Popular posts from this blog

1 Mwokozi umeokoa

138 Tukutendereza Yesu (Luganda)

7 Ni tabibu wa karibu