11 Nina haja nawe


1. Nina haja nawe
Kila saa;
Hawezi mwingine
Kunifaa.
 
Yesu, nakuhitaji
Vivyo kila saa!
Niwezeshe, Mwokozi,
Nakujia.
 
2. Nina haja nawe;
Kaa nami,
Na maonjo haya,
Hayaumi.
 
3. Nina haja nawe;
Kila hali,
Maisha ni bure,
Uli mbali.
 
4. Nina haja nawe,
Nifundishe
Na ahadi zako
Zifikishe.
 
5. Nina haja nawe,
Mweza yote,
Ni wako kabisa
Siku zote. 

Comments

Popular posts from this blog

1 Mwokozi umeokoa

138 Tukutendereza Yesu (Luganda)

7 Ni tabibu wa karibu