142 Babangu kule mbiguni.


1. Babangu kule mbinguni,
aliye juu pa malaika,
aangalia njia zangu
na kunilinda maisha.
 
2. Hata unywele kichwani
hauanguki ovyo tu
na siri zote za moyoni
zajulikana kwa Baba.
 
3. Zamani nisipojua,
amekwisha kuandika
mkononi mwake jina langu,
ndio upedo wake mkuu.
 
4. Ee Baba yangu u mwema,
nami nataka kufanya
kama malaika wafanyavyo
mbinguni kwako milele!.

Comments

Popular posts from this blog

1 Mwokozi umeokoa

138 Tukutendereza Yesu (Luganda)

7 Ni tabibu wa karibu