137 Yesu mponya


1. Yesu ndiye mganga wetu
Aponya wagonjwa wote;
Mganga wetu ni Yesu,
Aponyaye hasira. 
 
Tumsifu huyo Yesu
Tumsifu milele,
Kwani Mponya mtakata
Mwokozi wa wanyonge
 
2. Mganga wetu ni Yesu
Huondoa matusi;
Mganga wetu ni Yesu,
Mwenye kuponya choyo.
 
3. Mganga wetu ni Yesu
Huponya wivu wetu;
Yesu ndiye aponyae
Kelele za nyumbani.
 
4. Mganga wetu ni Yesu
Mponya wa tamaa mbaya;
Mganga wetu ni Yesu
Uasherati hufuta
 
5. Mganga wetu ni Yesu
Aponya kiu cha pombe,
Mganga wetu ni Yesu
Kila dhambi uponya

Comments

Popular posts from this blog

1 Mwokozi umeokoa

138 Tukutendereza Yesu (Luganda)

7 Ni tabibu wa karibu